Thursday, April 25, 2013

BRAZIL YAZOMEWA NA MASHABIKI WAKE.

TIMU ya taifa ya Brazil imejikuta ikizomewa na mashabiki wake wenyewe baada ya kujikuta wakitoka sare ya kufungana mabao 2-2 na Chile katika mechi ya kwanza ya kirafiki katika uwanja utakaotumika kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2014. Mechi hiyo iliyochezwa katika uwanja mpya uliofanyiwa ukarabati wa Mineirao uliopo jijini Horizonte ni ya mwisho kwa kocha Luis Felipe Scolari kabla ya kutaja kikosi cha mwisho Mei 14 kwa ajili ya michuano ya Kombe la Shirikisho Juni mwaka huu. Pamoja na mashabiki wengi wapatao 53,000 kujitokeza katika mchezo huo, walionyesha kutofurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa baada ya Chile kuonekana wakimiliki mpira zaidi ya wenyeji wao. Mshambuliaji nyota wa Brazil, Neymar akihojiwa mara baada ya mchzo huo amesema hali ya kuzomewa na mashabiki wao wameshaizoea na wanaichukulia hali hiyo kama changamoto.

No comments:

Post a Comment