Thursday, April 25, 2013

MWAMUZI AANGUKA UWANJANI NA KUFA BURKINABE.

MWAMUZI wa Burkina Faso ameanguka na kufariki dunia jana jijini Ouagadougou wakati akifanyiwa vipimo vya afya. Mwamuzi huyo Ouangraoua Moumouni ambaye pia alikuwa katibu mkuu wa Chama cha Waamuzi wa nchi hiyo-UNAF , alikuwa akifanyiwa majaribio yaliyoandaliwa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka la Burkina Faso-FBF alianguka uwanjani wakati zoezi hilo likiendelea. Mwamuzi huyo mwenye umri wa miaka 38 alitangazwa amekufa muda mchache baadae wakati akipatiwa huduma ya kwanza uwanjani hapo lakini familia yake ilikataa uchunguzi wa mwili wake na kuamua kumzika siku hiyohiyo. Moumouni kwa kawaida amekuwa akisimamia mechi za Ligi Kuu nchini Burkina Faso pamoja na zile za mashindano ya Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF.

No comments:

Post a Comment