Thursday, April 25, 2013

MBABE WA MADRID AWA LULU ULAYA.


MUDA mchache baada ya kuiangamiza Real Madrid kwa kufunga mabao manne, mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Robert Lewandowski amekuwa ‘almasi’ baada vilabu mbalimbali kujaribu kuiwinda sahihi yake. Vilabu hivyo ni pamoja na Bayern Munich na Manchester United ambao wameanza kuhaha kila kona ili kuhakikisha wanamnasa nyota huyo mapema. Mabao manne aliyofunga dhidi ya Real Madrid, yamemfanya aweke rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kuifunga timu hiyo ya Hispania mabao manne katika mechi ya ligi ya mabingwa. United wangekuwa wa kwanza kumpata nyota huyo lakini meneja wake Alex Ferguson akataka kuwe na subira lakini Bayern ambao wamenyakuwa ubingwa wa Ujerumani wanaonekana ndio wenye nafasi kubwa ya kumpata kwasasa.

No comments:

Post a Comment