Friday, April 26, 2013

SUAREZ KAONYESHA MFANO MBAYA - CAMEROON.

WAZIRI mkuu wa Uingereza, David Cameroon amesema mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez amenyesha mfano mbaya kwa kumng’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic. Suarez tayari amepewa adhabu ya kufungiwa mechi 10 na Chama cha Soka cha Uingereza kwa tukio hilo. Akihojiwa katika kipindi kikoja cha radio nchini Uingereza, Cameroon amesema akiwa kama baba na binadamu hadhani kama wanapaswa kutoa adhabu kali wakati mchezaji akifanya vitendo kama hivyo. Waziri mkuu huyo aliendelea kusema kuwa ni jambo linaloeleweka kama jopo la FA likikutana kutoa adhabu hiyo litamchukulia mchezaji huyo kama kioo cha jamii hivyo kutoa adhabu hiyo ili iwe mfano na kwa nyota wengine ambao vijana wadogo huwaiga kutokana na mafanikio waliyopata. Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers amedai kuwa kauli hiyo ya Cameroon ndio imepelekea Suarez kupewa adhabu kubwa ingawa waziri mkuu huyo alipinga vikali akidai kuwa amesema hivyo kama baba anayetizama soka.

No comments:

Post a Comment