Friday, April 26, 2013

WATU WANAPASWA WATUHESHIMU BADALA YA KUTUPONDA - INIESTA.

KIUNGO wa klabu ya Barcelona, Andres Iniesta amesisitiza kuwa watu hawaitendei haki timu hiyo baada ya kufungwa na Bayern Munich mabao 4-0 katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Watu ambali mbalimbali wamekuwa wakiponda kiwango cha timu hiyo baada ya kupigo hicho cha kushtusha walichikipata katika Uwanja wa Allianz Arena Jumanne huku wengi wengi wao wakidai enzi za timu hiyo kung’ara zimekwisha. Hata hivyo Iniesta amesisitiza kuwa ni mapema mno kudai kuwa kiwango cha timu hiyo kimekwisha na kuwataka watu wawape heshima zaidi kwasababu wanastahili. Iniesta amesema katika kipindi cha misimu mitano wameshinda taji la Ligi ya Mabingwa mara tatu na kufika zaidi ya mara tatu nusu fainali na kwasasa wanakaribia kunyakuwa taji la nne la ligi na kwao hayo ni mafanikio makubwa. Nyota huyo aliendelea kusema kuwa badala ya watu kuwaponda wanatakiwa wawaheshimu kwasababu wamekuwa wakijitolea kwa kila kitu pindi wanapokuwa uwanjani na wamefanikiwa mambo mengi. Barcelona inatarajiwa kukwaana na Athletico Bilbao baadae leo katika mchezo wa La Liga .

No comments:

Post a Comment