Friday, April 26, 2013

WAPUUZI WACHACHE HAWAWEZI KUNIFANYA NIONDOKE ITALIA - BOATENG.

KIUNGO wa klabu ya AC Milan, Kevin-Prince Boateng amesisitiza kuwa ana furaha kuwepo klabuni hapo na kuongeza kuwa matukio ya kibaguzi ambayo yamekuwa yakimuandama katika siku za karibuni hayawezi kumfanya aondoke Italia. Boateng mwenye umri wa miaka 26 kwa mara nyingine tena amekuwa mhanga wa mambo kibaguzi wakati timu yake ilipopoteza mchezo wa Serie A dhidi ya Juventus mwishoni mwa wiki iliyopita. Hata hivyo kiungo huyo wa kimataifa wa Ghana ameweka wazi kuwa hawezi kuruhusu kikundi kidogo cha watu kimfanye aondoke Italia. Boateng amesema anajisikia vyema kuwapo Milan na anachukulia kama nyumbani kwake hivyo atakaa hapo kwa kipindi kirefu kijacho. Amesema kuna kipindi alikuwa akifikiria kuondoka lakini amemua kubaki na hatarajii kwenda kokote kwasababu ya kikundi kidogo cha wapuuzi.

No comments:

Post a Comment