Saturday, April 27, 2013

ERIKSSON ATUMA CV ZAKE KUOMBA KIBARUA CAMEROON.

SHIRIKISHO la Soka nchini Cameroon-Fecafoot limebainisha kuwa majina makubwa akiwemo kocha wa zamani wa Uingereza Sven-Goran Erikkson wanafikiriwa kupewa kibarua cha kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo. Msemaji wa Fecafoot, Junior Binyam amesema kuwa wamepokea maombi zaidi ya 100 ya makocha mbalimbali wakitaka kibarua cha kuinoa timu hiyo inayaojulikana kwa jina la utani kama Indomitable Lions. Binyam amesema kuna baadhi ya makocha wa nyumbani lakini wengi walioomba ni makocha wa kigeni wakiwemo mchezaji wa zamani na kocha wa klabu ya Paris Saint-Germain Luis Fernandez, Eriksson, kocha wa timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC Claude Le Roy na kocha wa zamani wa Ufaransa Roger Lemerre. Katika majina hayo yote yatateuliwa majina matatu ambayo yatapelekwa kwa waziri wa michezo wan chi hiyo kwa ajili ya uteuzi rasmi wa atakayechukua nafasi hiyo ambayo iliachwa wazi na Jean Paul Akono aliyetimuliwa kutokana na mwenendo mbovu wa timu hiyo.

No comments:

Post a Comment