Thursday, May 30, 2013

FRENCH OPEN: SERENA NA VENUS WILLIAMS WAJITOA MASHINDANO YA WAWILI WAWILI.

WANADADA nyota katika mchezo wa tenisi, Serena na Venus Williams wamejitoa katika michuano ya wazi ya Ufaransa kwa wachezaji wawili wawili kabla ya kucheza hata mechi moja. Wanadada hao walitarajiwa kushiriki katika michuano hiyo kwa mara ya kwanza toka mwaka 2010 lakini walijitoa Jumatano na hakuna sababu yoyote iliyotolewa na waandaaji wa michuano hiyo. Mapema Venus alidai kusumbuliwa na matatizo ya mgongo wakati alipopoteza mchezo wake wa Jumapili iliyopita kwa kufungwa seti tatu wakati Serena yeye alifanikiwa kumlipizia kisasi dada yake na kutinga katika mzunguko wa tatu wa michuano hiyo. Nyota hao wawili wamefanikiwa kushinda jumla ya mataji 13 ya Grand Slam kwa michezo ya wawili wawili kwa wanawake yakiwemo mataji ya michuano ya wazi ya Ufaransa mwaka 1999 na 2010.

No comments:

Post a Comment