Thursday, May 30, 2013

NEYMAR KUTAMBULISHWA RASMI JUMATATU.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Brazil na klabu ya Santos, Neymar ambaye amesaini mkataba wa miaka mitano na Barcelona ya Hispania, anatarajiwa kutambulishwa rasmi Jumatatu. Akiongea na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Ufundi wa Barcelona Alberto Parreira amesema kwa Neymar amepewa ruhusa kwenda Barcelona baada ya kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Uingereza Jumapili. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 ambaye jina lake kamili ni Neymar da Silva Santos Junior alibainisha Jumanne kuwa ana hamu kubwa ya kujiunga na Barcelona lakini kwasasa anataka kufikiria zaidi michuano ya Kombe la Shirikisho inayotarajiwa kuanza mwezi ujao. Kombe la Shirikisho ni michuano ambayo hufanyika mwaka mmoja kabla ya kuanza rasmi michuano ya Kombe la Dunia na itaanza kutimua vumbi rasmi kuanzia Juni 15 hadi 30 mwaka huu. Brazil wamewahi kunyakuwa Kombe la Dunia mara tani na Kombe la Shirikisho mara tatu.

No comments:

Post a Comment