Thursday, May 30, 2013

PELLEGRINI, CITY WAKARIBIA KUFUNGA "NDOA".

MENEJA wa klabu ya Malaga aliyebwaga manyanga, Manuel Pellegrini amesema anamatumaini makubaliano ya awali waliyofikia na klabu ya Manchester City yatakamilika. Pellegrini ambaye ni raia wa Chile amesema ana majukumu ya kuipa kipaumbele Manchester City kwani wameshafanya mazungumzo ya awali na ni mategemeo yake yatakwenda vyema. Wiki iliyopita kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 ambaye amewahi pia kuzinoa klabu za Villarreal na Real Madrid alitangaza kuondoka Malaga mwishoni mwa msimu huu baada ya kuinoa klabu hiyo kwa miaka miwili na nusu. Kocha huyo amekuwa akihusishwa na tetesi za kipindi kirefu za kuhamia City toka klabu hiyo ilipomtimua kocha wake Roberto Mancini mapema mwezi huu.

No comments:

Post a Comment