Thursday, May 30, 2013

BALE AMEZALIWA KUITUMIKIA MADRID - PEREZ.

RAIS wa klabu ya Real Madrid, Florentino Perez ameongeza uvumi wa kutaka kumsajili mshambuliaji nyota wa klabu ya Tottenham Hotspurs Gareth Bale baada ya kusisitiza kuwa nyota amezaliwa kwa ajili ya kuichezea klabu hiyo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 amefunga mabao 21 katika Ligi Kuu nchini Uingereza msimu huu mabao ambayo yameifanya Spurs kukosa kidogo nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa na anategemewa kusainishwa mkataba mpya ambao utamuwezesha kulipwa paundi 130,000 kwa wiki msimu ujao. Hatahivyo wakala wa mchezaji huyo Jonathan Barnett alikiri mapema jana kuwa mshambuliaji huyo anaweza kukubali ofa yoyote watakayotoa Madrid. Perez aliongeza uvumi huo kwa kauli yake ya kudai kuwa mchezaji huyo kawazaliwa kwa ajili ya kuichezea klabu yake huku mkurugenzi mpya wa michezo wa Zinedine Zidane naye akimtaka mchezaji huyo baada ya kumfananisha na Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.

No comments:

Post a Comment