Thursday, May 30, 2013

STOKE CITY WAMPA KIBARUA HUGHES.

KLABU inayoshiriki Ligi Kuu nchini Uingereza, Stoke City imemteua Mark Hughes kuwa meneja mpya wa klabu hiyo baada ya kutimuliwa Queens Park Rangers-OPR. Hughes amechukua nafasi ya Tony Pulis ambaye aliondoka Stoke kwa maelewano wiki iliyopita baada ya kuifundisha klabu hiyo kwa kipindi cha miaka saba. Hughes mwenye umri wa miaka 49 ambaye pia amewahi kuifundisha Manchester City amekaa bila toka alipoondoka QPR Novemba mwaka jana. Kocha huyo raia wa Wales alishindwa kupata ushindi katika mechi 12 za ligi kwenye msimu wa 2012-2013 na kupelekea kutimuliwa QPR na nafasi ya kuchukuliwa na Harry Redknapp.

No comments:

Post a Comment