Wednesday, May 29, 2013

CRUYFF AMSHAURI VILANOVA KUJIUZULU UKOCHA KWA MUDA.

NGULI wa zamani wa soka wa Barcelona, Johan Cruyff amemshauri meneja wa klabu hiyo Tito Vilanova kujiuzulu wadhifa huo na kufikiria zaidi kuhusu mustakabali wa afya yake. Vilanova mwenye umri wa miaka 44 aliondolewa uvimbe wa saratani katika koo lake mwaka 2011 lakini Desemba mwaka jana hali hiyo ilijirudia tena hivyo kumfanya kukosa miezi kadhaa katika msimu wa 2012-2013 wakati akipata matibabu. Kocha huyo alirejea katika benchi la ufundi la Barcelona Aprili mwaka huu lakini Cruyff anafikiri ingekuwa vyema kwa manufaa yake kama angeachana na masuala ya ukocha kwasasa. Cruyff amesema hasemi hayo kwa kumkosea heshima ila ni kwa manufaa yake kwani huwezi kufundisha katika kiwango cha juu kama afya yako haiku vizuri.

No comments:

Post a Comment