Wednesday, May 29, 2013

BALE NI GHALI ZAIDI YA NEYMAR - WAKALA.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Gareth Bale amedai kuwa itawagharibu Real Madrid zaidi ya fedha ambazo Barcelona imelipa kwa ajili ya Neymar kama wanataka kumsajili nyota huyo raia wa Wales. Wakala huyo Jonathan Barnett amesema inashangaza lakini gharama yoyote iliyogharimu Barcelona kumsajili, Bale ana thamani zaidi ya hiyo. Rais wa Madrid Florentino Perez anahisiwa kumhitaji nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 ikiwa ni hatua ya kwanza ya kukibadilisha kikosi cha timu hiyo baada ya kumaliza masimu vibaya kwa kushindwa kunyakuwa taji lolote. Madrid walimkosa Neymar baada ya mahasimu wao Barcelona kuwazidi na kumnyakuwa nyota huyo kwa mkataba wa miaka mitano mwishoni mwa wiki iliyopita hivyo kuhamishia nguvu zao kwa Bale. Lakini Barnett amedai kuwa Bale ni mchezaji bora zaidi ya Neymar hivyo kama Madrid wanamhitaji hawana neno wanawasubiri ila itawagharimu kiasi kikubwa.

No comments:

Post a Comment