Wednesday, May 29, 2013

HENRY AITAKA ARSENAL KUWEKA MALENGO YA MBALI ZAIDI.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu ya Arsenal, Thierry Henry ameionya klabu hiyo kuwa lazima waongeze malengo yao kuliko kufikiria kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kila msimu. Kikosi cha Arsene Wenger kilishangilia baada ya kujihakikishia nafasi ya nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Newcastle United katika mechi ya mwisho na kupelekea wadau mbalimbali kuiponda timu hiyo. Henry ambaye kwasasa anacheza katika klabu ya New York Red Bulls amesema kitu pekee ambachi kinaweza kushangiliwa katika msimu huu ni kitendo cha kuwa nyima nafasi mahasimu wao Tottenham Hotspurs nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa. Henry amesema kama ukiwa mshabiki wa kweli wa Arsenal lazima ufurahie kuwashinda mahasimu wenu lakini bado klabu hiyo ina changamoto ya kuhakikisha inarejesha heshima yake kwa kushinda vikombe.

No comments:

Post a Comment