Wednesday, May 29, 2013

TOURE AKAMILISHA USAJILI HURU KWENDA LIVERPOOL.

KLABU ya Liverpool imebainisha kuwa wamekubali kumsajili beki wa kimataifa wa Ivory Coast Kolo Toure wakati mkataba wake na Manchester City utakapomalizika Julai mosi mwaka huu. Beki huyo mwenye umri wa miaka 32 alijiunga na City akitokea Arsenal ada ya paundi milioni 16 mwaka 2009 ambapo mwaka mmoja baadae aliungana na mdogo wake Yaya aliyetokea Barcelona. Kolo Toure alikuwa amekabidhiwa mikoba ya unahodha wa City lakini alipoteza nafasi yake ya kikosi cha kwanza baada ya kufungiwa miezi sita kwa kosa la kukutwa na chembechembe za dawa zilizokatazwa michezoni Machi 2011. Mchezaji huyo alidai kuwa alitumia vidonge vya kupunguza uzito vua mke wake na alikuwa hajui kwamba vidonge hivyo vina dawa ndani yake zilizokatazwa. Pamoja na kufungiwa huko Toure anaondoka City akiwa na medali za Kombe la FA na Ligi Kuu ya Uingereza.

No comments:

Post a Comment