Wednesday, May 29, 2013

KAMATI YA BLATTER YATUPILIA MBALI AJENDA YA KIKOMO CHA UONGOZI NA UMRI.

KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA iliyokuwa ikiongozwa na rais wake Sepp Blatter wametupilia mbali pendekezo la kikomo cha umri na muda wa uongozi kuwa ajenda ya kuzungumziwa katika mkutano wake Ijumaa. Uamuzi huo ambao umekuwa ukizua mjadala karibu kipindi cha mwaka mzima juu ya kikomo cha umri kwa viongozi wa juu ulikubaliwa na kamati hiyo iliyokutana katika kisiwa cha Bahari ya Hindi. Hatua imekuja ikiwa ni siku moja baada ya Blatter ambaye anaweza kugombea tena nafasi hiyo katika kipindi cha miaka miwili ijayo kwa sheria za sasa, kudai kuwa kuweka kikomo cha umri kutachukuliwa kama aina ya ubaguzi. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa FIFA imedai kuwa ajenda mbili za kikomo cha umri na muda wa kukaa madarakani zimeondolewa kwa ajili ya kujadiliwa zaidi ambapo zinaweza kuletwa tena katika mkutano mkuu wa shirikisho hilo 2014.

No comments:

Post a Comment