Wednesday, May 29, 2013

EURO MILIONI 60 ZAMPELEKEA FALCAO MONACO.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao yuko mbioni kukamilisha uhamisho wake unaogharimu kiasi cha euro milioni 60 kutoka Atletico Madrid kwenda klabu ya AS Monaco ya Ufaransa. Falcao mwenye umri wa miaka 27 amekuwa gumza katika kipindi hiki cha usajili huku vilabu mbalimbali vikubwa kama Real Madrid, Chelsea na Manchester City zikipigana vikumbo kutaka saini yake. Hata hivyo, badala ya kwenda huko nyota huyo sasa atatua Monaco baada ya kusaini mkataba wa miaka minne na klabu hiyo jana. Falcao tayari amekamilisha vipimo vya afya mapema wiki hii na kitu kilichobakia ni utambulisho rasmi kwa klabu hiyo ambao utafanyika muda wowote. Nyota huyo anakuwa mchezaji wan ne kusajiliwa na Monaco katika kipindi hiki cha majira kiangazi baada ya Joao Moutinho na James Rodriguez kutoka Porto ambao wameigharimu klabu hiyo jumla ya euro milioni 70 pamoja na Rocardo Carvalho wa Madrid.

No comments:

Post a Comment