Wednesday, May 29, 2013

COLE AKABIDHIWA UNAHODHA WA MUDA LEO.

BEKI wa kushoto wa klabu ya Chelsea, Ashley Cole atakabidhiwa unahodha wa timu ya taifa ya Uingereza katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Jamhuri ya Ireland kama heshima ya kufikisha mechi ya 100 akiitumikia nchi yake. Meneja wa Uingereza Roy Hodgson aliwaambia waandishi wa habari kuwa Cole ndiye atakayekiongoza kikosi chake lakini Frank Lampard anataendelea kuwa nahodha wakati Steven Gerrard hayupo. Hodgson amempongeza nyota huyo kwa kuwa mtumishi bora sio kwa klabu za Arsenal na Chelsea lakini pia kwa taifa lake. Cole atatimiza mechi ya 102 akiwa na timu ya taifa kwenye mchezo huo utakaochezwa Wembley baadae leo ambapo anakuwa mchezaji wa saba wan chi hiyo kufikisha idadi hiyo ya michezo.

No comments:

Post a Comment