Tuesday, May 28, 2013

ZIDANE MKURUGENZI MPYA WA MICHEZO MADRID - PEREZ.

RAIS wa klabu ya Real Madrid, Florentino Perez amedai kuwa Zinedine Zidane atakuwa mkurugenzi mpya wa michezo wa klabu hiyo. Akihojiwa na kituo kimoja cha redio nchini Hispania, Perez amesema hajui nani atakuwa kocha mpya wa klabu hiyo kuchukua mikoba ya Jose Mourinho waliositisha mkataba wake lakini anajua wazi kwamba Zidane ndiye atakuwa mkurugenzi wa michezo. Zidane mwenye umri wa miaka 40 ameichezea Madrid katika kipindi cha mwa mwaka 2001 na 2006 na kurejea tena miaka miwili iliopita kama mshauri wa Perez. Perez alikataa kuzungumzia juu ya makocha wawili Carlo Ancelotti na Jupp Heynckes wanaopewa nafasi kubwa kuchukua mikoba ya Mourinho akidai kuwa suala hilo litawekwa wazi wiki ijayo.
WAKATI HUOHUO
RAIS wa klabu ya Real Madrid, Florentino Perez anajiandaa kumfanya Cristiano Ronaldo kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani ili kumbakisha katika klabu hiyo baada ya kuondoka kwa Jose Mourinho. Perez amesema angependa kumfanya Ronaldo kuwa ghali zaidi duniani na watafanya kila linalowezekana ili kuhakikisha anakuwa na furaha. Nyota huyo wa zamani wa Manchester United amekuwa akihusishwa na tetesi za kurejea Old Trafford katika kipindi cha majira ya kiangazi huku pia mabingwa wa Ufaransa, Paris Saint-Germain nao wakimmezea mate. Ronaldo amekuwa akiifungia mabao mengi Madrid toka alipotua kwa ada ya paundi milioni 80 mwaka 2009 akifunga mabao 146 katika mechi 135 alizochezea klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment