Tuesday, May 28, 2013

NEYMAR ANGETUGHARIMU EURO MILIONI 150 - PEREZ.

RAIS wa klabu ya Real Madrid, Florentino Perez amebainisha kuwa Neymar angewagharimu kiasi cha euro milioni 150 kama wangefanikiwa kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Brazil. Madrid walikuwa na nia ya kumsajili Neymar mwenye umri wa miaka 21 katika kipindi cha msimu wa 2013-2014 lakini nyota huyo aliamua kukaa kwenda huko na badala yake kusaini kwa mahasimu wao Barcelona. Perez amesema walikuwa na nafasi kubwa ya kumsajili nyota huyo miaka mitatu iliyopita lakini kumekuwa na hali tofauti katika kipindi hiki na ingewagharimu kiasi hicho kama wangefanikiwa. Rais huyo wa Madrid alikwenda mbali zaidi na kutoa maoni yake kuwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Cristiano Ronaldo ni mchezaji bora wa dunia ingawa alikiri kuwa asingesita kumsajili nyota wa Barcelona Lionel Messi kama angepata nafasi.

No comments:

Post a Comment