Thursday, May 30, 2013

MAN UNITED, MAN CITY ZAMGOMBEA FABREGAS.

KLABU za Manchester United na Manchester City zinashindana kumrejesha katika Ligi Kuu kiungo nyota wa klabu ya Barcelona Cesc Fabregas msimu ujao. Meneja mpya wa United David Moyes amepanga kumtengea nyota huyo kitita cha paundi milioni 25 kiungo huyo baada ya Barcelona kuonyesha nia ya kumuuza nahodha huyo wa zamani Arsenal. Lakini mahasimu wa United, timu ya City nao walipata tetesi za kutaka kuuzwa kwa nyota huyo wa kimataifa wa Hispania na wao pia kuanza kumnyatia. Arsenal ndio wenye nafasi ya kwanza kwenye usajili wa nyota huyo ikiwa ni sehemu ya makubaliano na Barcelona, lakini Moyes kwa kipindi kirefu amekuwa akimhusudu kiungo huyo mwenye umri wa miaka 26 na kuna kipindi alitaka kumpeleka Everton kwa mkopo wakati akichipukia.

No comments:

Post a Comment