Thursday, May 30, 2013

ABIDAL ATANGAZA KUONDOKA BARCELONA.

BEKI wa kushoto nyota wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Barcelona, Eric Abidal ametangaza kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu ikiwa ni miezi miwili imepita tangu arejee uwanjani baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuandikiza ini. Abidal aliwaambia waandishi wa habari kuwa pamoja na kuondoka klabuni hapo lakini atarejea tena katika nafasi tofauti, baada ya tetesi kuwa timu hiyo imempa kibarua kuendesha shule ya michezo. Huku akibubujikwa na machozi Abidal amesema angependa kuendelea kuichezea Barcelona lakini klabu hiyo inaangalia mambo tofauti na lazima aheshimu hilo. Abidal mwenye umri wa miaka 33 ambaye upasuaji wake wa kupandikiza ini ulifanikiwa kwa kiwango cha kushangaza na kurejea uwanjani mwezi uliopita, mkataba wake unaishia mwishoni mwa msimu huu. Pamoja na kuondoka Barcelona nyota huyo amesema ataendelea kucheza kwa kipindi kingine kifupi katika klabu yoyote itakayomsajili.

No comments:

Post a Comment