Friday, May 31, 2013

PLATINI AWAPASHA FIFA.

RAIS wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA, Michel Platini anaamini kuwa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA haliko tayari kuweka kikomo cha umri na muda wa uongozi kwa viongozi wa juu baada ya kutupilia ajenda hiyo kwenye mkutano wake mkuu. Rais wa FIFA Sepp Blatter alitupilia mbali ajenda hiyo kwa kudai kuwa inatengeneza ubaguzi miongoni mwa viongozi lakini Platini amedai kuwa suala hilo limewachukiza viongozi wengi wa kamati ya utendaji ya FIFA. Platini amesema miongozi mwa wajumbe 24 wa kamati ya utendaji saba kati yao ambao wanaiwakilisha UEFA hawakufurahishwa na hatu hiyo. Platini aliendelea kusema kuwa suala hilo limekuwa likijadiliwa kwa kipindi cha miaka miwili lakini FIFA wanaonekana kama hawakubaliani nalo ndio maana wanalipiga danadana.

No comments:

Post a Comment