Friday, May 31, 2013

LEONARDO AFUNGIWA MIEZI TISA.

MKURUGENZI wa Michezo wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG, Leonardo amefungiwa miezi tisa kujishughulisha na masuala ya michezo kwa kosa la kumsukuma mwamuzi. Leonardo alionekana katika picha za video akimsukuma mwamuzi Alexandre Castro kwa bega lake baada ya kukasirishwa na kitendo cha Thiago Silva kupewa kati nyekundu katika mchezo ambao PSg ilitoa sare ya bao 1-1 na Valenciennes. Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 43 alikana kufanya tukio hilo huku PSG ikithibitisha kumkatia rufani kupinga adhabu hiyo. Mbali na adhabu hiyo ya Leonardo, PSG nao pia wamekatwa alama tatu adhabu ambayo wataitumikia msimu ujao wa Ligi Kuu nchini Ufaransa.

No comments:

Post a Comment