Friday, May 31, 2013

GUTI AMPONDA MOURINHO.

KIUNGO wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Guti amemshambulia Jose Mourinho kwa kudai kuwa Mreno huyo alitakiwa kuonyesha unyenyekevu zaidi kufuatia timu yake kushindwa kunyakuwa taji lolote msimu wa 2012-2013. Madrid walishuhudia mahasimu wa Barcelona wakinyakuwa taji la Ligi Kuu wakati wao wakipata kipigo kutoka kwa majirani zao Atletico Madrid kwenye fainali ya Kombe la Mfalme hatua ambayo imepelekea Mourinho kuondoka mwishoni mwa msimu. Guti amesema walikuwa wakitegemea vitu vingi kutoka kwake na sio mataji pekee, lakini wakati unapomaliza msimu vibaya inabidi uonyeshe unyenyekevu kidogo ili kuwapoza mashabiki. Nyota huyo amesema hakuwepo kujua ni kitu gani gani kinaendelea katika vyumba vya kubadilishia nguo kila siku lakini kama una mkataba wa miaka minne halafu unaondoka kabla ya kumaliza mkataba huo lazima kutakuwa na tatizo. Pamoja na kumaliza msimu huu vibaya Mourinho amefanikiwa kuingoza Madrid kunyakuwa taji moja la ligi, Kombe la Mfalme na Kombe la Ligi katika kipindi cha miaka mitatu ambayo ameinoa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment