Friday, May 31, 2013

FIFA YAPITISHA SHERIA KALI KWA WABAGUZI.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limepigia kura adhabu mpya kwa ajili ya vitendo vya kibaguzi ambapo timu zinaweza kushushwa daraja au kutolewa katika mashindano kama wakikutwa na hatia ya kufanya vitendo hivyo. Adhabu ya kwanza kwa matukio hayo itakuwa ni onyo, kutozwa faini au kuchezeshwa kaika uwanja mtupu wakati adhabu ya pili kama tukio hilo likijirudia itakuwa ni kukatwa alama, kuenguliwa katika mashindano au kushushwa daraja. Rais wa FIFA Sepp Blatter anaamini kuwa hatua inatuma ujumbe madhubuti kwa watu wenye tabia za kibaguzi kwamba muda wao umeisha. Azimio la kupambana na vitendo vya kibaguzi lilipigiwa kura ya kupitishwa kwa asilimia 99 katika mkutano mkuu wa FIFA unaofanyika huko Mauritius.

No comments:

Post a Comment