Friday, May 31, 2013

VALDES KUBAKIA BARCELONA MPAKA 2014.

GOLIKIPA wa klabu ya Barcelona, Victor Valdes amesisitiza kuwa hataki kuondoka klabuni hapo katika kipindi cha usajili na badala yake ameamua kukaa mpaka mkataba wake utakapomalizika Juni mwaka kesho. Mapema msimu huu Valdes aliiambia klabu hiyo kwamba hahitaji kuongeza mkataba wake hivyo kuzusha tetesi kuwa anaweza kuondoka mwishoni mwa msimu huu. Klabu iliyopanda daraja msimu huu ya AS Monaco ndiyo iliyoaminika kuwa inataka kusajili nyota huyo lakini mwenyewe sasa ameweka wazi nia yake ya kumaliza mkataba wake akiwa Camp Nou. Valdes amesema nafasi anayocheza imekuwa na changamoto nyingi na anahisi kama amechoka kiakili ndio maana amemua kumaliza mkataba wake 2014 bila kuongeza mwingine ili aweze kupumzika.

No comments:

Post a Comment