Sunday, May 26, 2013

SISI NI KIZAZI CHA DHAHABU CHA BAYERN - LAHM.

BEKI wa kati wa kimataifa wa Ujerumani na klabu ya Bayern Munich, Philipp Lahm anaamini kuwa ushindi wa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya unakifanya kikosi cha timu hiyo kuwa kizazi cha dhahabu. Bayern ambao wanajulikana pia kama The Bavarians walishindwa mara mbili katika hatua ya fainali ya michuano hiyo katika kipindi cha misimu mitatu iliyopita lakini bao la ushindi la dakika ya 89 lililofungwa na Arjen Robben liliwahakikishia ushindi mabao 2-1 dhidi ya wajerumani wenzake Borussia Dortmund. Lahm anaamini ushindi huo waliopata katika Uwanja wa Wembley utakuwa chachu ya kufanya vizuri zaidi katika mchezo wao mwingine wa fainali ya Kombe la Ujerumani itakayofanyika Juni mosi katika Uwanja wa Allianz Arena huku tayari wakiwa wameshanyakuwa taji la Bundesliga. 
Nyota huyo aliendelea kusema kuwa kama mchezaji unahitaji kuweno katika kizazi cha dhahabu unatakiwa kushinda mataji makubwa na anashukuru walifanya hilo jana.

No comments:

Post a Comment