Sunday, May 26, 2013

NEYMAR KUSAINI MKATABA WA MIAKA MITANO BARCELONA.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Brazil, Neymar amesema kuwa anatarajia kusaini mkataba wa miaka mitano na klabu ya Barcelona ya Hispania Jumatatu. Neymar alichagua Barcelona na kuwatema mahasimu wao Real Madrid baada ya klabu yake ya Santos kumaliza utata wa kumng’ang’ania mchezaji huyo kwa kipindi cha miaka mitatu na kumwachia kuondoka kabla ya michuano ya Kombe la Dunia 2014. Nyota huyo alithibitisha hayo katika ukurasa wake wa mtandao wa Instagram na Twitter kwamba atasaini mkataba wa miaka mitano kesho huku klabu ya Santos kwenye ukurasa wake wa facebook na katika mtandao wa Barcelona wote wakithibitisha uamuzi huo wa Neymar. Neymar aliongeza kuwa familia na marafiki zake tayari wote wanajua kuhusiana na uamuzi wake huku akiwashukuru mashabiki wa Santos kwa kuwa pamoja naye katika kipindi cha miaka tisa ambayo amekuwepo hapo.

No comments:

Post a Comment