Saturday, May 25, 2013

ADEBAYOR AITWA TOGO.

KOCHA wa timu ya taifa ya Togo, Didier Six amemuita mshambualiaji nyota na nahodha wan chi hiyo Emmanuel Adebayor katika kikosi chake ambacho kinakabiliwa na mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia dhidi ya Cameroon Juni 9 na Libya Juni 16 mwaka huu. Mshambuliaji huyo anayecheza katika klabu ya Tottenham Hotspurs hakutokea mara ya mwisho alipoitwa na kocha huyo kwa ajili ya mchezo dhidi ya Cameroon uliochezwa Machi mwaka huu. Adebayor amekuwa katika mzozo na kocha huyo raia wa Ufaransa ambaye amedai kuwa ndio alikuwa chanzo cha nchi hiyo kung’olewa katika michuano ya Mataifa ya Afrika yaliyofanyika Afrika Kusini 2013. Six pia amemuita golikipa Kossi Agassi ambaye amekuwa katika mzozo na Shirikisho la Soka nchini humo kuhusiana na masuala ya posho. Togo kwasasa inashika nafasi ya pili katika kundi I wakipisha alama moja na Cameroon ambao wanaongoza kundi hilo wakifuatiwa na Libya alama tano na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo alama nne.

No comments:

Post a Comment