Monday, May 27, 2013

ZIDANE APEWA KIBARUA CHA KUHAKIKISHA BALE ANATUA MADRID.

MMOJA wa wachezaji bora kabisa kuwahi kuitumikia klabu ya Real Madrid, Zinedine Zidane amepewa kazi ya kuhakikisha anamshawishi mshambuliaji nyota wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Gareth Bale ili aweze kusajili na klabu hiyo. Gazeti la Marca nchini Hispania limeripoti kuwa nyota huyo wa zamani ndio mshauri mkuu kuhusiana na suala la Bale ana anajaribu kumshawishi raia wa Madrid Florentino Perez kuwa lazima waipate saini ya nyota huyo. Kwa kuonyesha kwamba hawataki mchezo kwenye suala hilo Madrid wamepania hata kutoa kitita cha paundi milioni 65 kwa ajili ya kumchukua Bale kutoka Spurs. 
Zidane kwa kipindi kirefu amekuwa akimhusudu nyota huyo wa kimataifa wa Wales akidai kuwa amekuwa akiitazama Tottenham kwa ajili ya Bale ukiachilia mbali Ronaldo na Messi ambao ndio wachezaji anaowahusudu duniani kwa hivi sasa. Zidane ameendelea kufafanua kwa kummwagia sifa Bale kwamba ni mchezaji aliyekamilika na amekuwa akifunga mabao mazuri na muhimu ana kasi, mbunifu na anavutia kumtizama.

No comments:

Post a Comment