Monday, May 27, 2013

LEWANDOWSKI BAYERN INAMHUSU - WAKALA.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa klabu ya Borussia Dortmund, Robert Lewandowski amesema kuna uwezekano mkubwa wa mshambuliaji huyo kujiunga na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya Bayern Munich. Hata hivyo, wakala huyoaitwaye Cezary Kucharski aliiambia luninga moja nchini Ujerumani kwamba Bayern bado hawajafikia makubaliano ya mambo binafsi ya nyota huyo wa kimataifa wa Poland. Wakala huyo aliendelea kusema kuwa wao wako tayari lakini badi hawajasaini chochote kwasababu klabu nayo inatakiwa iafiki makubaliano hayo. Bayern ambao ni mabingwa wapya wa Ujerumani tayari wamemnyakuwa kiungo wa Dortmund Mario Gotze mwenye umri wa miaka 20 kwa ada ya euro milioni 37.

No comments:

Post a Comment