Monday, June 24, 2013

ARSHAVIN MBIONI KUTUA ZENIT.

NAHODHA wa zamani wa timu ya taifa ya Urussi, Andrei Arshavin anategemewa kukamilisha taratibu za kurejea klabu yake ya zamani ya Zenit Saint Petersburg baada ya kuitumikia Arsenal kwa muda wa miaka mitano. Klabu hiyo ndio ilimuibua nyota huyo mwenye miaka 32 sasa wakati akiwa kinda kabla ya Arsenal kumuona na kumyakuwa. Arshavin ambaye alitua Zenit kwa mkopo kwa muda wakati wa msimu wa pili wa 2011-2012 kwasasa yuko huru baada ua kuachwa na Arsenal mwishoni mwa msimu huu. Nyota likuwemo katika kikosi cha Zenit kilichonyakuwa taji la Europa League mwaka 2008 na pia katika kikosi cha Urusi kkilichoshiriki michuano ya Ulaya 2008 kabla ya kwenda Arsenal.

No comments:

Post a Comment