Saturday, June 22, 2013

BOLT AFUZU MICHUANO YA DUNIA.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica, Usain Bolt amefanikiwa kufuzu kushiriki mbio za mita 100 za dunia kwa kushinda michuano ya mchujo iliyofanyika nchini kwake kwa kutmia muda wa sekunde 9.94. Katika mbio hizo Bolt alianza taratibu lakini aliongeza kasi zaidi alipofikia mita 50 na kumkumpita Nickel Ashmeade na kujihakikishia nafasi ya kwenda jijini Moscow katika michuano ya dunia ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Agosti 10 mpaka 18. Mjamaica mwingine mkali katika mbio Yohan Blake yeye alishindwa kushiriki mbio za kuvuzu za mita 200 kwasababu ya majeraha lakini atashiriki mbio za mita 100 kama bingwa mtetezi baada ya Bolt kuenguliwa katika mbio hizo kwenye michuano ya dunia iliyofanyika jijini Daegu mwaka 2011. Kwa upnde wa Marekani nyota wa mbio hizo Tyson Gay naye amefanikiwa kukata tiketi ya kwenda Moscow baada ya kumshinda Justin Gatlin katika mbio za mita 100 kwa kutuimia muda wa sekunde 9.75 ukiwa ni muda wake wa haaka zaidi kwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment