Saturday, June 22, 2013

PSG YAMCHUKUA BLANC KUZIBA PENGO LA ANCELOTTI ANAYETAKA KUONDOKA.


KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG imefikia makubaliano na Laurent Blanc ili aje kuwa meneja mpya wa klabu hiyo ambao ndio mabingwa wa Ligi Kuu nchini Ufaransa maarufu kama Ligue 1 msimu uliopita. Blanc mwenye umri wa miaka 45 amekaa bila kibarua toka alipoacha kuinoa timu ya taifa ya Ufaransa kufuatia kuenguliwa katika hatua ya robo fainai katika michuano ya Ulaya mwaka jana. Blanc ambaye alikuwa beki enzi zake akicheza soka amewahi kufundisha katika klabu ya Bordeaux kuanzia mwaka 2007 mpaka 2010 na kuisaidia timu hiyo kunyakuwa taji la Ligue 1 mwaka 2009. Hatua hiyo ya PSG imekuja kufuatia kocha wa sasa wa klabu hiyo Carlo Ancelotti kuomba kuondoka baada ya kuinoa kwa miezi 18 huku kukiwa na tetesi kuwa anataka kwenda Real Madrid ya Hispania.

No comments:

Post a Comment