Saturday, June 22, 2013

MCHEZAJI WA CROATIA AFIA UWANJANI.

MCHEZA soka wa Croatia Alen Pamic mwenye umri wa miaka 23 ameanguka ghafla na kufariki uwanjani wakati mchezo ukiendelea. Mchezaji huyo ambaye alikuwa kicheza katika klabu ya NK Istra 1961 inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo amekuwa na hitoria ya matatizo ya moyo na ameshawahi kuanguka zaidi ya mara tatu katika kipindi cha nyumba kabla ya kufariki. Februari mwaka huu alianguka na kupoteza fahamu katika mechi baina ya timu yake dhidi ya timu ya Lokomotiva lakini pamoja na tatizo hilo alisisitiza kuendelea kucheza soka na daktari alimruhusu. Pamic ni mtoto wa mchezaji wa kimataifa wa zamani wan chi hiyo aitwaye Igor ambaye kwasasa ndiye kocha wa Istra.

No comments:

Post a Comment