Sunday, June 23, 2013

FORLAN NA WENZAKE WACHELEWA MAZOEZINI KWA KUKWAMA KWENYE LIFTI BRAZIL.

MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya taifa ya Uruguay, Diego Forlan na wachezaji wenzake wawili wa tmu hiyo wamekumbwa na kadhaa ya kukwama katika lifti ya hoteli waliyofikia kwa zaidi ya dakika 30 kitendo ambacho kilipelekea kuchelewa kuanza kwa mazoezi ya timu hiyo ili kujiwinda na mchezo wao wa mwisho wa Kombe la Shirikisho unaotarajiwa kupigwa leo. Forlan, Diego Perez, Sebastian Eguren pamoja na mmoja wa viongozi wa benchi la ufundi walikuwa wakishuka chini kutoka ghorofa ya saba kwenye hoteli hiyo iliyopo jijini Recife lakini ilikwama ghafla na kushindwa kufanya kazi. Perez alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai walikwama kwa zaidi ya nusu sasa lakini walikuwa wanaweza kupumua vizuri na mwanga wa kutosha ulikuwepo ndani ya lifti hiyo. Uruguay inatarajia kumaliza mchezo wake wa mwisho wa kundi B na timu vibonde ya Tahiti baadae leo katika mji huo uliopo kaskazini mwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment