Sunday, June 23, 2013

SHARAPOVA AMPONDA WILLIAMS KWA KAULI YAKE.

MWANADADA nyota katika tenisi anayeshika namba mbili katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanawake, Maria Sharapova amemponda hasimu wake Serena Williams na kuchunga kauli zake kwa kutoropoka hovyo. Williams kutoka Marekani ambaye ni bingwa mtetezi wa michuano ya Wimbledon ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho hivi karibuni alilazimika kuomba radhi kwa kauli aliyoitoa kuhusiana na kesi ya ubakaji inayomhusu msichana wa miaka 16 huko jijini Ohio. Sharapova ambaye ni raia wa Urusi amesema amesikitishwa na kauli aliyotoa Williams ambaye anashika namba moja katika orodha kuhusiana na kesi hiyo. Williams alimfunga Sharapova na kutwaa ubingwa wa michuano ya wazi ya Ufaransa mapema mwezi huu na wawili hao hawawezi kukutana mapema katika michuano ya Wimbledon mpaka fainali.

No comments:

Post a Comment