Sunday, June 23, 2013

BOLT AJITOA MASHINDANO YA OSTRAVA.

MWANARIADHA nyota wa Jamaica, Usain Bolt ametangaza kujitoa katika mashindano ya Golden Spike yaliyokuwa yafanyike Juni 27 jijini Ostrava, Jamhuri ya Czech, na badal yake ameamua kubakia nyumbani na kufanya mazoezi zaidi. Katika taarifa yake aliyotoa mapema leo, Bolt aliwaomba radhi mashabiki wake wa Ostrava kwa kutokwenda huko kushiriki mbio hizo na badala yake anataka kuongeza juhudi zaidi katika mazoezi akiwa na kocha wake nchini Jamaica kabla ya kusafiri kwenda Ulaya. Katika mbio za Ostrava Bolt alikuwa amepangwa kukimbia katika mbio za mita 400 kupokezana vijiti pamoja na nyota mwingine wa Jamaica, Yohan Blake ambaye naye alijitoa mapema kutokana na majeraha. Bolt, Blake, Michael Frater na Nesta Carter walifanikiwa kuweka rekodi mpya ya dunia katika mbio hizo kwa kutumia muda wa sekunde 36.84 katika mashindano ya olimpiki yaliyofanyika jijini London, Uingereza mwaka jana.

No comments:

Post a Comment