Sunday, June 23, 2013

JAPAN INAHITAJI KUWA NA WACHEZAJI WENGI ZAIDI KATIKA LIGI KUBWA - HONDA.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Japan, Keisuke Honda anaamini kuwa wachezaji wengi zaidi wa timu ya taifa ya nchi hiyo wanahitaji kucheza katika ligi kubwa duniani baada ya timu hiyo kupata kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mexico na kuenguliwa katika michuano ya Kombe la Shirikisho inayoendelea nchini Brazil. Mabao mwili ya Mexico yaliyofungwa na Javier Hernandez yalitosha kuwapa ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa kundi A na kufanikiwa kusonga mbele pamoja na bao la dakika za majeruhi la kufutia machozi la Japan lililofungwa na Shinji Okazaki. Na baada ya kipigo hicho Honda ambaye anakipiga katika klabu ya CSKA Moscow ya Urusi anaamini kuwa wachezaji wenzake wanahitaji kutafuta timu katika vilabu vikubwa dunia ili waweze kupata uzoefu utakaowawezesha kuongeza ushindani zaidi katika timu hiyo. Honda amesema walifungwa na Italia ambao walipata siku mbili pekee za mapumziko hivyo wanahitaji akili na nguvu kama hizo kushinda katika hali yoyote na hayo yanaweza kutokea kama wachezaji wa nchi hiyo watacheza katika vilabu vikubwa.

No comments:

Post a Comment