Monday, June 24, 2013

MWAMUZI AKIRI KUWAPA ITALIA BAO LA MDONDO.

SHIRIKISHO la Soka Dunia-FIFA limedai kuwa mwamuzi Ravshan Irmatov amekiri kuwapa Italia bao pili kwa makosa wakati wa mchezo wa Kombe la Shirikisho baina ya timu hiyo na Brazil ambao wenyeji walishinda kwa mwabao 4-2. Bao lililofungwa na Giorgio Chiellini lilikubaliwa ingawa mwamuzi alishapuliza filimbi kuashiria penati kwenda kwa Italia kitendo ambacho kiliwaudhi wachezaji wa Brazil na kuzonga mwamuzi juu ya uwamuzi wake huo. FIFA imesema kuwa mwamuzi huyo wa Uzbekstan baadae alikiri kufanya kosa hilo na kukiri kupuliza filimbi kuashiria penati. Lakini pamoja na kukiri kutenda kosa kwa mwamuzi huyo FIFA hawajathibitisha kama watamrudisha nyumbani au ataendelea kuchezesha mechi za nusu fainali ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment