Monday, June 24, 2013

HONG MYUNG-BO KOCHA MPYA KOREA KUSINI.

CHAMA cha Soka cha Korea Kusini kimteua nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya nchi hiyo, Hong Myung-bo kuwa kocha mpya wa timu hiyo. Hong ambaye alikuwa nahodha katika kikosi kilichoshika nafasi ya pili kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2002 iliyofanyika nchini kwao amechukua nafasi ya Choi Kang-hee ambaye amebwaga manyanga baada ya kuisadia nchi hiyo kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2014 kwa mara ya nane mfululizo. Hong alikua kocha wa kikosi cha nchi hiyo ambacho kilinyakuwa medali ya fedha kwenye michuano ya olimpiki iliyofanyika London mwaka jana ambapo kwa kipindi kirefu alitegemewa kuteuliwa wadhfa huyo. Choi alichukua mikoba ya kuinoa nchi hiyo mwaka 2011 na kipindi alidai kuwa kazi yake kubwa ni kuhakikisha wanapata nafasi ya kwenda Brazil kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2014 na baada ya hapo angejiuzulu.

No comments:

Post a Comment