Friday, June 21, 2013

PIRLO KUIKOSA BRAZIL.

KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Italia, Andrea Pirlo anatarajiwa kukosa mchezo wa mwisho wa kundi A dhidi ya wenyeji Brazil kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kupata majeraha ya msuli katika mguu wake wa kulia. Kocha wa viungo wa nchi hiyo, Enrico Castellacci amesema anamatumaini Pirlo anaweza kurejea katika mechi ya nusu fainali lakini ukijumuisha na kukosekana kwa Daniele De Rossi ambaye naye pia atakosa mchezo wa mwishoni itabidi kocha wa timu hiyo Cesar Prandelli abadili kikosi chake. Italia ilitinga hatua ya nusu fainali baada ya kuibugiza Japan ka mabao 4-3 na kufikisha alama sawa na Brazil katika kundi lao ambapo mechi ya mwisho ndio itakayoamua nani atasonga mbele kama mshindi wa kundi. Timu zote mbili itabidi zipange vikosi vyao kamili ili kutafuta ushindi na kuepuka kukutana na bingwa wa dunia Hispania katika hatua ya nusu fainali.

No comments:

Post a Comment