Friday, June 21, 2013

MARCEDES WAFUNGIWA KUFANYA MAJARIBO MSIMU HUU.

TIMU ya Marcedes imefungiwa kufanya majaribio kwa madereva wake chipukizi kwa mwaka huu pamoja na kupewa onyo kali kwa kosa la kufanyia majaribio magurudumu ya Pirelli kinyume cha utaratibu. Kampuni hiyo ya magurudumu ya Pirelli nayo pia imepewa onyo kwa kutumia gari jipya linalotumiwa katika mashindano ya langalanga na dereva Lewis Hamilton katika majaribio ya siku tatu waliyofanya nchini Hispania mwezi uliopita. Kamati maalumu ya uchunguzi wa suala hilo iliyoundwa na Chama cha Kimataifa cha Langalanga-FIA kilichukua hatua hiyo baada ya kuwakuta Mercedes na hatia ya kutenda kosa hilo ambalo ni kinyume cha utaratibu wa mashindano hayo. Katika sheria za langalanga timu yoyote hairuhusiwi kufanya majaribio magurudumu kwa zaidi ya kilometa 1000 pindi msimu wa mshindano hayo unapoanza na hata wakifanya majaribio hayo hawapaswi kutumia gari zao mpya zinazotumika katika msimu husika.

No comments:

Post a Comment