Friday, June 21, 2013

MMOJA AFA KATIKA MAANDAMANO BRAZIL.

RAIS wa Brazil, Dilma Rousseff ameitisha mkutano wa dharura leo ikiwa ni siku moja baada ya muandamanaji kuuwawa na wengine zaidi ya milioni 1.25 wakiendelea kuandamana nchi nzima wakidai huduma nzuri kwa jamii. Pilikapilika hizo za uandamanaji ambazo mara nyingine zinaleta vurugu kubwa, zinafanyika wakati nchi hiyo iikiwa mwenyeji wa michuano ya Kombe la Shirikisho inayoendelea ambayo huchezwa mwaka mmoja kabla ya Kombe la Dunia. Raia wengi wa Brazil wamekuwa wakigadhabika juu ya gharama kubwa za maandalizi zilizotumika kwa ajili ya kuandaa na Kombe la Dunia 2014 na michuano ya olimpiki kipindi cha kiangazi itakayofanyika jijini Rio de Janeiro 2016.  Jijini Rio polisi wamekuwa wakipambana na waandamanaji hao ambao hujikusanya karibu na Uwanja wa Maracana ambapo wamekuwa wakilazimika kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto ili kuwatawanya.

No comments:

Post a Comment