Saturday, June 22, 2013

PRANDELLI AOMBA RADHI KWA KAULI YAKE DHIDI YA BALOTELLI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Italia, Cesar Prandelli ameomba radhi kwa kauli yake aliyosema juu ya mshambuliaji nyota wa klabu Mario Balotelli akidai kuwa nyota huyo alikuwa mchezaji pekee aliyeruhusiwa kutoka hotelini kwasababu ni mweusi. Washauri wa mambo ya kiusalama waliwaambia wachezaji wan chi hiyo kutotoka hotelini wakati maandaano yakiendelea kurindima katika michuano hiyo ya Kombe la Shirikisho. Prandelli amesema nyota huyo nayekipiga katika klabu ya AC Milan aliruhusiwa kutoka kwasababu rangi yake ni tofauti na wachezaji wenzake lakini baadae aliomba radhi na kudai kuwa alikuwa akitania. Balotelli aliruhusiwa kutoka hotelini kwa ajili ya kwenda kufanya shughuli za kijamii kuwasaidia watoto wanaotoka katika sehemu masikini katika mji wa Salvador nchini Brazil. Italia inatarajiwa kukwaana baadae leo na wenyeji wa michuano hiyo Brazil ili kutafuta bingwa wa kundi lao kabla ya kwenda katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment