Wednesday, June 26, 2013

RONALDO AZIDI KUWATIA TUMBO JOTO MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ureno, Cristiano Ronaldo anaweza kuwa njiani kurejea Manchester United kutokana na tetesi kuwa atafanya mazungumzo na viongozi wa Old Traford katika siku tatu zijazo. Nyota huyo wa klabu ya Real Madrid amekuwa akihusishwa na tetesi za kurejea Uingereza baada ya kuonekana kukosa furaha huko Santiago Bernabeu lakini inaaminika kwamba ujio wa Carlo Ancelotti unaweza kushawishi kubakia nchini Hispania. Gazeti moja nchini Hispania liliripoti kuwa Ronaldo ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Ureno atakutana na viongozi hao wa United kabla ya kurejea Madrid kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi. Meneja mstaafu wa United Sir Alex Ferguson katika kipindi cha karibuni amekuwa akimfukuzia Ronaldo ambaye inaaminika kutaka nafasi ya kuiwakilisha klabu hiyo ambayo ndiyo iliyomtengeneza mpaka kuwa mmoja wa wachezaji bora duniani. Rais wa Madrid Florentino Perez amenyesha kuwa na uhakika wa nyota huyo mwenye thamani ya paundi milioni 80 kusaini mkataba mwingine ambao utambakisha nchini humo lakini Ronaldo alikanusha habari hizo katika mitandao ya kijamii.

No comments:

Post a Comment