Wednesday, June 26, 2013

NEYMAR HAWEZI KUMFUNIKA MESSI BARCELONA - SYLVINHO.

BEKI wa zamani wa klabu ya Barcelona, Sylvinho anaamini kuwa Neymar atapata wakati mgumu wa kumfunika Lionel Messi kufuatia uhamisho wake kutoka klabu ya Santos kwenda kwa mabingwa hao wa Ligi Kuu nchini Hispania. Mambo makubwa yanategemewa ka mshambuliaji huyo nyota wa kimataifa wa Brazil kufuatia kiwango bora anachokionyesha katika michuano ya Kombe la Shirikisho lakini Sylvinho anafikiri Neymar mwenye miaka 21 anaweza kuishia kucheza nyuma ya Messi kwenye klabu hiyo. Sylvinho anakiri kuwa Neymar ni mchezaji wa wachezaji bora kabisa kwasasa lakini suala la kumfunika Messi ambaye ameshinda tuzo nne za Ballon d’Or litakuwa suala gumu sana. Beki huyo aliendelea kusema kuwa kumekuwa na wachezaji wengi nyota wa Brazil kama Ronaldo, Romario na Ronaldinho lakini wote hao hawajapata kufikia kiwango alichonacho Messi kwasasa. Sylvinho amewahi kushinda mataji matatu ya La Liga na mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Barcelona katika kipindi cha kuanzia mwaka 2004 mpaka 2009.

No comments:

Post a Comment