Wednesday, June 26, 2013

WIMBLEDON: FEDERER AKATAZWA KUVAA RABA ZAKE, AZARENKA AJITOA.

MCHEZAJI nyota wa tenisi Roger Federer kutoka Switzerland amekatazwa kutovaa viatu vyake ambavyo vina soli ya rangi ya chungwa baada ya kuonekana kama amevunja sheria za michuano ya Wimbledon ambayo wachezaji wanatakiwa kuvaa mavazi meupe kuanzia juu mpaka viatu. Federer mwenye umri wa miaka 31 bingwa mara saba wa michuano hiyo alikuwa amevaa viatu hivyo wakati wa mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo aliocheza Jumatatu. Katika sheria za michuano ya Wimbledon wachezaji wote ambao wanashiriki michuano hiyo wanatakiwa kuvaa mavazi meupe hata kama wakiwa katika mazoezi. Wakati huohuo mwanadada nyota katika mchezo huo anayeshika namba mbili katika orodha za ubora duniani Victoria Azarenka amelazimika kujitoa katika michuano hiyo dakika chache kabla ya kuanza kwa mchezo wake wa mzunguko wa pili. Azarenka raia wa Belarus ambaye ni bingwa wa michuano ya wazi ya Australia aliumia goti lake la kulia katikati ya mchezo wa mzunguko wa kwanza dhidi ya Maria Jaoo Koehler wa Portugal lakini alifanikiwa kuendelea na kushinda mchezo huo.

No comments:

Post a Comment